Gospel Movie Video Swahili "Ivunje Laana" (3) - Je, Neno la Mungu Lipo Isipokuwa Biblia?

  • 6 years ago
Baadhi ya watu wa kidini huamini kuwa maneno na kazi zote za Mungu ziko katika Biblia, na kwamba hakuna maneno na kazi ya Mungu isipokuwa yale yaliyo katika Biblia. Je, aina hii ya mtazamo inaafikiana na ukweli? Biblia inasema, "Na kuna mambo mengi pia aliyoyafanya Yesu, ambayo, kama yakiandikwa kila moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa." (Yohana 21:25)." Mwenyezi Mungu alisema, “Kile Mungu alicho na anacho milele hakiishi wala hakina mipaka. Mungu ni chanzo cha uhai na vitu vyote. Mungu hawezi kueleweka na kiumbe yeyote aliyeumbwa. Mwishowe, ni lazima bado Nimkumbushe kila mtu: Msimwekee Mungu mipaka katika vitabu, maneno, au tena katika matamshi Yake yaliyopita. Kuna neno moja tu kwa sifa ya kazi ya Mungu—mpya. Hapendi kuchukua njia za zamani au kurudia kazi Yake, na zaidi ya hayo Hapendi watu kumwabudu kwa kumwekea mipaka katika upeo fulani. Hii ndiyo tabia ya Mungu” (Neno Laonekana katika Mwili).

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Injili ya Kushuka kwa Ufalme: https://sw.kingdomsalvation.org/
Kanisa la Mwenyezi Mungu: https://sw.godfootsteps.org/
Kanisa la Mwenyezi Mungu YouTube: https://www.youtube.com/channel/UCkUDnudSY6_KR123N2Yr7mw
Kanisa la Mwenyezi Mungu Facebook: https://www.facebook.com/kingdomsalvationsw/
Kanisa la Mwenyezi Mungu Twitter: https://twitter.com/CAGchurchsw
Kanisa la Mwenyezi Mungu Instagram: https://www.instagram.com/thechurchofalmightygodsw/
Kanisa la Mwenyezi Mungu Vimeo: https://vimeo.com/thechurchofalmightygodsw
Kanisa la Mwenyezi Mungu Blogger: http://nikanisalamwenyezimungu.blogspot.com/
Google Play: https://play.google.com/store/apps/details?id=org.godfootsteps.thechurchofalmightygod
App Store: https://itunes.apple.com/ke/app/the-church-of-almighty-god/id1166298433

Barua Pepe: contact.sw@kingdomsalvation.org
Wasiliana Nasi: +254-700-427-192

Recommended